Daima Lyrics & Tabs by Eric Wainaina

Daima

guitar chords lyrics

Eric Wainaina

Album : Sawa SawaPlayStop

Umoja ni fahari yetu
Undugu ndio nguvu
Chuki na ukabila

Hatutaki hata kamwe
Lazima tuungane, tuijenge nchi yetu
Pasiwe hata mmoja
Anaetenganisha
Naishi, Natumaini,
Najitolea daima Kenya,
Hakika ya bendera
Ni uthabiti wangu
Nyeusi ya wananchi na nyekundu ni ya damu
Kijani ni ya ardhi, nyeupe ya amani
Daima mimi mkenya
Mwananchi mzalendo

Kijani ni ya ardhi, nyeupe ya amani
Daima mimi mkenya
Mwananchi mzalendo
Kwa uchungu na mateso
Kwa vilio na uzuni
Tulinyakuliwa Uhuru
na mashujaa wa zamani
Hawakushtushwa na risasi
au kufungwa gerezani
Nia yao ukombizi kuvunja pingu za ukoloni
Naishi, Natumaini,
Najitolea daima Kenya,
Hakika ya bendera
Ni uthabiti wangu
Nyeusi ya wananchi na nyekundu ni ya damu
Kijani ni ya ardhi, nyeupe ya amani
Daima mimi mkenya
Mwananchi mzalendo
Wajibu wetu
Ni Kuishi kwa upendo
Kutoka ziwa Mpaka pwani
Kaskazini na kusini
Naishi, Natumaini,
Najitolea daima Kenya,
Hakika ya bendera
Ni uthabiti wangu
Nyeusi ya wananchi na nyekundu ni ya damu
Kijani ni ya ardhi, nyeupe ya amani
Daima mimi mkenya
Mwananchi mzalendo

More tracks of "Eric Wainaina"

Like us on Facebook.....
-> Loading Time :0.0330 sec